Na Mwandishi Wetu, Nairobi
Pamoja na kuonekana ameshuka kiwango wakati akiwa Yanga,
Moses Odhiambo ni kati ya wachezaji walioipa Gor Mahia ubingwa wa Kenya baada
ya kuukosa kwa miaka 13.
Odhiambo amekuwa akiendelea kutumika kama mmoja wa
wachezaji wakongwe na wenye msaada mkubwa.
Akizungumza na SALEHJEMBE jijini hapa, Odhiambo alisema
amekuwa akiendelea kufanya vizuri kwa kuwa anaijua kazi yake.
“Watu wakisema umeshuka wewe ukaamini, basi unakwisha. Lakini
mimi sikuamini hilo, nikaendelea kujituma na kufanya mambo yangu.
“Sasa ni kati ya wachezaji ambao tumeweka rekodi ya kuipa
Gor ubingwa ilioukosa kwa miaka 13, kitu ambacho kwetu ni kikubwa sana,”
alisema Odhiambo aliyewahi kukipa Simba na baadaye Yanga.
0 COMMENTS:
Post a Comment