Picha inaonyesha wajumbe wawili wa
kamati ya usajili ya Yanga, Seif Ahmed ‘Magari’ na Abdallah Bin Kleb lazima
kuna jambo.
Hapa walikuwa wanafuatilia mechi ya
kirafiki jana, kati ya Taifa Stars dhidi ya Future Taifa Stars kwenye Uwanja wa
Karume jijini Dar es Salaam.
Wawili hawa wanajulikana kwa makali yao
kwenye usajili, wakiingia kwenye 18, basi asilimia 95 ni bao na hapa walikuwa
kwenye 18.
Tayari wameanza makali yao kwa kumsajili
Juma Kaseja ambaye Simba walisema hana kiwango, sasa imeelezwa wanawania kati
ya washambuliaji kutoka Ruvu Shooting (Elias Maguri), Mtibwa Sugar (Juma Luizio)
au Mbeya City (Mwagano Yeya).
Lakini inawezekana ni danganya toto,
kumbe wamemlenga mwingine kabisa. Macho hayo manne huenda yameangalia kwingine.
Tusubiri.
0 COMMENTS:
Post a Comment