Ismail Aden Rage amemteua Michael
Wambura katika kamati ya utendaji ya Simba.
Pamoja na hivyo, amempa nafasi ya Mjumbe
wa Bodi ya Wadhamini, Rahma Al Kharusi maarufu kama Malkia wa Nyuki.
Nafasi ya kamati hiyo ilikuwa ya Malkia wa
nyuki lakini amempeleka na kuwa mjumbe wa bodi ya wadhamini.
Wambura amewahi kuwa katibu mkuu wa
Simba na ndiye alikuwa mtu wa kwanza kumshinda Rage katika nafasi ya ukatibu mkuu wa Chama cha Soka Tanzania (FAT).
0 COMMENTS:
Post a Comment