Selemani Matola ndiye kocha msaidizi mpya
wa Simba anayechukua nafasi ya Jamhuri Kihwelo ‘Julio’.
Uongozi wa Simba umethibitisha hilo leo
kwamba Matola ndiye atasaidiana na Kocha Mkuu mpya, Zdravko Logarusic kutota Croatia.
Uongozi wa Simba umethibitisha hilo
ikiwa ni dakika chache baada ya kuwatimua kibaruani Abadallah Kibadeni
aliyekuwa kocha mkuu na msaidizi wake, Julio.
Katika kipindi hiki, Matola amekuwa
akifanya kazi ya kukinoa kikosi cha Simba B ambacho kinashiriki michuano ya
Uhai.
0 COMMENTS:
Post a Comment