Mshambuliaji mkongwe, Gaudence Mwaikimba na beki wa pembeni, Malika
Ndeule, wametangazwa kuwa huru baada ya kumalizana na Azam FC.
Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo zinaeleza kuwa wachezaji hao
wamemalizana na klabu hiyo, kuhusu kuendelea kubaki klabuni hapo itategemea na ujio
wa kocha mpya atakayefika hivi karibuni kuchukua nafasi ya Stewart Hall.
“Mwaikimba na Ndeule ndiyo wachezaji pekee ambao mikataba yao inatarajiwa
kumalizika mwanzoni mwa Desemba, mwaka huu, hivyo wapo huru kufanya mazungumzo
na klabu yoyote itakayowahitaji.
“Lakini sidhani kama watabaki, mfano Mwaikimba ni mchezaji mzuri
lakini umri nao umeenda sana, lakini kama akipata timu nyingine bado anao uwezo
wa kucheza katika ligi kuu,” kilisema chanzo hicho.
0 COMMENTS:
Post a Comment