Mashabiki
wa Simba wameshinda katika michezo yote ya Bonanza ililofanyika kwenye Uwanja
wa Shule ya Msingi Uwanja wa Ndege Morogoro, jana.
Katika
michezo hiyo, walishinda mechi ya kwanza ambapo waliibuka washindi kwa
kuwafunga mashabiki wav Yanga mabao 2-1 kwa njia ya mikwaju ya penati.
Aliyeanza
kufunga ni Josephat Matiko na la pili lilifungwa na, Omary Masho, ambapo Yanga
walipata walipata bao moja mfungaji akiwa ni Khalfan Semika.
Katika
mechi ya pili, Simba waliendeleza ubabe baada ya kuwafunga tena Yanga kwa mabao
4-3, walioifungia Simba ni Isihaka Pedo alifunga mawil na mawili mengine
yalifungwa na Majidi Mussa kwedakika ya 30 na 41.
Kipindi cha pili ambapo magoli ya Yanga yalifungwa na Omary Chipo, Omary Said na Mapunda Cheche.
Pia Simba waliendeleza ushindi kwa kuwatesa wapinzani wao kwa kuwazidi nguvu katika uvutaji kamba na hata kukimbiza kuku pia simba walishinda.
0 COMMENTS:
Post a Comment