Kocha wa makipa wa Taifa Stars, Juma Pondamali amesema hataki tena
kuwa kocha wa makipa na badala yake anataka kuwa kocha mkuu au msaidizi katika
ngazi ya klabu.
Pondamali ambaye ni kocha wa makipa wa Coastal Union amesema kuwa kwa
sasa kazi hiyo ataifanya akiwa kwenye timu ya taifa pekee hadi hapo baadaye
atakapopata ajira anayoitaka.
“Nimeamua kutoendelea kuwa kocha wa makipa tena katika klabu za ligi
kuu, ninachohitaji ni kuwa kocha mkuu au msaidizi na siyo zaidi ya hapo, maisha
ni mabadiliko na mimi ninahitaji mabadiliko ambayo nimeamua,” alisema kocha
huyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment