HASHEEM KATIKA MOJA YA MECHI ZA NBA |
Timu ya Oklahoma City Thunder
anayoitumikia Mtanzania Hasheem Thabeet imepoteza mchezo wake wa ugenini dhidi
ya Los Angeles Clippers.
Clippers walifanikiwa kushinda kwa
pointi 111-103 za wageni hao ambao walionekana kama wangeshinda huku
mshambuliaji wao, Kelvin Durant akionekana kuwa msumbufu zaidi.
Katika mechi hiyo ya NBA iliyochezwa
jana jijini Los Angeles, wenyeji walikuwa nyuma katika vipindi vyote viwili
hadi mapumziko.
Lakini wakacharuka katika vipindi viwili
vya mwisho na kufanikiwa kusawazisha kabla ya kutangulia na baadaye kuibuka na
ushindi.
Thabeet ambaye ni Mtanzania na pekee
kutokea Afrika Mashariki anayecheza katika ligi hiyo maarufu alicheza kwa zaidi
ya dakika 15 katika mchezo huo.
FINAL
OKC | ||
LAC |
33 | 29 | 16 | 25 | 103 |
25 | 28 | 30 | 28 | 111 |
0 COMMENTS:
Post a Comment