Mshambuliaji nyota wa Simba, Amissi Tambwe amesema
bado ana kazi ya kufanya na Simba.
Tambwe raia wa Burundi amesema angependa kubaki Simba
na kuendelea kufanya kazi.
“Lakini kama kutakuwa na makubaliano kati ya Simba
na klabu nyingine, pia ninaweza kwenda.
“Lakini napenda kucheza ligi ya Tanzania angalau
msimu mmoja nikiwa pale na Simba,” alisema.
Hata hivyo, Tambwe hakutaka kuzungumzia zaidi
kuhusiana na Simba, hali iliyoonyesha huenda kuna tatizo.
“Sasa kidogo kuhusu Simba nisingependa kuzungumza zaidi
ya hapa,” alisema.
Kumekuwa na taarifa timu kadhaa zimeonyesha nia ya
kumchukua Mrundi huyo anayeongoza kwa kupiga mabao ligi kuu, ana bao 10.
Hata hivyo, tayari uongozi wa Simba umeishasema
hauna mpango wa kumuuza na kuwataka wanaomuania waachane na wazo hilo.
0 COMMENTS:
Post a Comment