Hali ya winga nyota wa zamani wa Yanga
na Simba, Edibily Lunyamila imeimarika kwa jioni hii.
Lunyamila amelazwa katika hospitali ya
Mwananyamala jijini Dar kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo.
Taarifa zilizotufikia punde, Lunyamila
anaendelea vizuri ukilinganisha na mchana.
Mashine za msaada wa kupumua
zimeondolewa na sasa anaweza kupumua mwenyewe.
Ndugu yake wa karibu amesema kuna nafuu
ingawa bado hali yake haijaiamarika sana.
“Bado haijawa nzuri sana lakini sasa ni
afadhari,” alisema.
Lunyamila ambaye sasa ni mchambuzi wa
masuala ya soka katika gazeti la CHAMPIONI ameanza kusumbuliwa na presha hivi
karibuni.
Mwanasoka huyo aliyechipukia kisoka
mkoani Shinyanga ingawa ni mwenyeji wa Kigoma alikuwa akisifika kwa kasi na
mashuti makali wakati anakimbia na mpira lakini krosi za maana.
0 COMMENTS:
Post a Comment