KASEJA AKITOKA UWANJANI BAADA YA MECHI DHIDI YA SIMBA |
Kipa mpya wa Yanga, Juma Kaseja,
amewaomba msamaha mashabiki wa timu hiyo baada ya kuruhusu mabao matatu kuingia
wavuni katika mechi ya Nani Mtani Jembe iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam.
Hii ilikuwa mechi ya kwanza kwa Kaseja
kucheza tangu atue kujiunga na timu hiyo kwenye usajili wa dirisha dogo
lililofungwa Desemba 15, mwaka huu akitokea Simba baada ya mkataba wake
kumalizika.
Tukio hilo la kuwaomba msahamaha
mashabiki wa Yanga, kipa huyo alilifanya mara baada ya mechi kumalizika, akitoka
kwenye vyumba vya kubadilishia nguo kuelekea kwenye basi la timu hiyo.
Wakati anaelekea kwenye basi hilo, kundi
kubwa la mashabiki wa timu hiyo lilimvamia Kaseja aliyekuwa amezungukwa na makomandoo
wa Yanga na kuhoji sababu za kufungwa mabao hayo.
0 COMMENTS:
Post a Comment