TAMBWE AKISHANGILIA BAADA YA KUIFUNGIA SIMBA BAO LA KWANZA |
Bao la kwanza la mshambuliaji wa kimataifa wa Simba, Amissi Tambwe, lilisababisha askari
wa usalama barabarani ‘traffic’ aliyekuwa na sare za kazi, kushangilia na
kuvunja kiti Uwanja wa Taifa, Dar kutokana na furaha iliyozidi.
Juzi,
Simba na Yanga zilicheza mchezo wa Nani Mtani Jembe, Simba ikashinda mabao 3-1,
lakini kuhusu shindano la vinywaji lililohusu mashabiki, Yanga ilijinyakulia Sh
milioni 98.4 wakati Simba ikipata Sh milioni 1.6, kati ya Sh milioni 100
zilizokuwa zikigombewa.
Baada ya Tambwe ambaye alipachika mabao mawili, kufunga bao la kwanza, traffic huyo
ambaye hakuweza kufahamika jina, alipagawa na kusababisha kuvunja kiti
alipokuwa akishangilia katika jukwaa la Simba.
Tambwe
alifanikiwa kupachika bao la kwanza dakika ya 13.
0 COMMENTS:
Post a Comment