December 14, 2013



 
Imefahamika kiungo mkongwe, Per Mertesacker alijikuta akimshambulia kwa maneno rafiki yake Mesut Ozil baada ya kuwaonyesha pozi mashabiki wa Arsenal.
 
Mara baada ya Arsenal kupokea kipigo cha mabao 6-3 kutoka kwa Man City, Mertesacker  na Ozil walizozana wakati wakitoka uwanjani.

Baadaye ilielezwa hali hiyo ilitokana na Mertesacker  kumlaumu Ozil kushindwa kuwashukuru mashabiki wa Arsenal waliosafiri kutoka London hadi Manchester katika mechi hiyo.


Ozil hakuonyesha kujali na alimjibu maneno yaliyoonyesha kumuudhi Mertesacker  ambaye alimfuata akionekana kuwa na hasira zaidi.
Baadaye Mertesacker  alirusha shati yake kwa mashabiki hao kuonyesha heshima kwao na kuthamini sapoti yao.


Kuhusiana na hilo, Wenger alisema: “Wajerumani wanajuana na usiwe na wasi, watalimaliza wenyewe.”

Mertesacker na Ozil wote ni wachezaji wa timu ya taifa ya Ujerumani, halafu washkaji kinoma.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic