Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi,
amesema yupo tayari kuifundisha Yanga kama kocha msaidizi iwapo atahakikishiwa
maslahi mazuri.
Mwambusi ambaye amefanikiwa kuipandisha
Mbeya City msimu huu na kucheza Ligi Kuu Bara amekuwa akiwindwa na Yanga kwa
ajili ya kuchukua nafasi ya Fred Felix Minziro.
Mwambusi amesema taarifa hizo hajazipata rasmi kutoka kwa viongozi wa mabingwa
hao watetezi wa ligi kuu lakini iwapo watamfuata atawasilikiza na kuwatajia dau
ambalo yeye anataka.
Alisema yeye kama kocha, kazi yake ni
kufundisha mpira, hivyo yupo tayari kwenda popote iwapo tu atapata maslahi
mazuri.
“Taarifa rasmi sijazipata lakini
wakinifuata nitaongea nao kwa kuwa tayari watakuwa wameonyesha kuniheshimu
kutokana na kazi ninayoifanya kukubalika kwao,” alisema Mwambusi.
0 COMMENTS:
Post a Comment