Kiungo wa Azam, Mcha Khamis 'Vialli', atakuwa nje
ya dimba kwa wiki moja akiuguza goti lake la kushoto aliloumia akiwa kwenye
kikosi cha timu ya taifa katika michuano ya Chalenji.
Daktari
wa Azam, Mwanandi Mwankemwa, alisema tayari kiungo huyo baada ya kutibiwa
ameanza mazoezi mepesi na atajiunga na wenzake baada ya wiki moja.
Alisema wachezaji wengine wote wapo fiti
wakijiandaa na Michuano ya Mapinduzi inayotarajiwa kufanyika Januari mwakani
mjini Zanzibar.
“Wachezaji wote wapo vizuri isipokuwa
Mcha ambaye ana tatizo la goti la kushoto aliloumia kwenye Michuano ya
Chalenji, nimempa wiki moja zaidi ili ajiunge kwenye mazoezi na wenzake,”
alisema Mwankemwa ambaye pia ni daktari wa timu ya taifa (Taifa Stars).
0 COMMENTS:
Post a Comment