Kocha Ernie Brandts rasmi ameachishwa
kazi ya kuinoa Yanga.
Kocha huyo raia wa Uholanzi amepewa
siku 30 ili awe ameondoka zake.
Lakini kwa kawaida ndiyo hatafanya
kazi Yanga kwa kuwa timu hiyo ina mambo mengi ya kufanya na haiwezi kusubiri.
Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya
Yanga, Abdallah Bin Kleb amewaambia waandishi leo makao makuu ya klabu hiyo
jijini Dar kwamba watamlipa Brandts kila kitu chake.
Gazeti la michezo la Championi ndiyo
lilikuwa la kwanza kuandika kuhusiana na taarifa hiyo leo asubuhi.
Brandts ameondoka Yanga baada ya
kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Yanga katika mechi ya Nani Mtani Jembe juzi
Jumamosi.
Hapo jana mwenyekiti wa club ya yanga alitangaza kwamba mechi ya nani mtani jembe ilikuwa ni bonanza lkn Hatimae bonanza lamfukuza kocha jangwani
ReplyDelete