MANJI AKIFUNGUKA |
Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji leo amemtolea uvivu
mzee maarufu wa klabu hiyo, Ibrahim Akilimali na kumtaka aache kuzungumza hovyo
kama vile kiongozi.
Manji amemueleza mzee Akilimali mbele ya wanachama
zaidi ya 400 waliojitokeza kwenye mkutano wa wanachama uliofanyika kwenye
Ukumbi wa PTA jijini Dar es Salaam.
MZEE AKILIMALI AKIMSIKILIZA MANJI |
Huku wengi wakiwa hawatarajii, Manji alimtaka mzee
Akilimali kufuata katiba na kuachana na kuzungumza mambo ilimradi.
“Mambo yamekuwa ni mengi, si sahihi kuzungumza kila
kitu, nakuheshimu sana na wewe ni mzee wangu.
“Lakini si sahihi kuzungumza tu bila ya ruhusa ya
uongozi, msemaji wa klabu ni mwenyekiti na kuna viongozi.
“Nimesema ninakuheshimu, nimekukuta Yanga,
umenipokea na kuniunga mkono na ndiyo maana leo niko hapa.
“Lakini nakueleza ukweli na ninaamini kwa kuwa
nimefanya utaelewa na kujirekebisha,” alisema Manji huku wanachama
wakimshangilia.
WAKIKUMBATIANA |
Baada ya hapo, Manji alikwenda kuzungumza na mzee
Akilimali, wakapeana mikono na kukumbatiana.
Baadaye Manji aliendelea na masuala mbalimbali
ikiwemo kuzungumzia mwenendo wa Yanga katika michuano mbalimbali.
Pamoja na hivyo, Manji alihimiza suala la nidhamu
kwa wanachama huku akisisitiza watakaokiuka, basi atawatimua mara moja.
0 COMMENTS:
Post a Comment