MESSI (KULIA) AKIWA KAZINI |
Washambuliaji Amissi Tambwe, Ramadhan
Singano ‘Messi’ na Haruna Chanongo, leo Jumatatu wanatarajiwa kuanza mazoezi
mepesi baada ya kutoka kwenye majeraha.
Wachezaji hao juzi Jumamosi walishindwa
kucheza kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Mtibwa kutokana na kusumbuliwa na
majeraha. Simba ilifungwa 1-0 katika mchezo huo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.
Daktari wa Simba, Yassin Gembe, alisema Tambwe alikuwa akisumbuliwa na nyama za
paja alizoumia mazoezini, Messi aliumia kidole gumba cha mkono kwenye mechi ya
fainali ya Kombe la Mapinduzi wakati Chanongo aliteguka kiganja cha mkono.
Alisema nyota hao leo Jumatatu watakuwa
na programu ya kufanya mazoezi mepesi kwenye Uwanja wa Kinesi, Shekilango
jijini Dar.
“Nina majeruhi watatu ambao ni Tambwe,
Singano na Chanongo, lakini wote wataanza mazoezi mepesi kesho (leo) tayari kwa
maandalizi ya mzunguko wa pili,” alisema Gembe.
0 COMMENTS:
Post a Comment