Kiongozi wa
zamani wa Simba, Juma Nkamia ametangazwa kuwa Naibu Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo.
Nkamia
ambaye ni Mbunge wa Kondoa Kusini (CCM),anachukua nafasi ya Amos Makala ambaye amehamia katika wizara nyingine ya maji.
Nkamia
aliyewahi kuwa Katibu Mwenezi wa Simba, ametangazwa leo wakati wa baraza jipya
la mawaziri ambalo limetangazwa baada ya baadhi ya mawaziri kufutwa kazi na
wengine.
Nkamia ambaye
taaluma yake ni mwandishi wa habari amewahi kufanya kazi ya utangazaji katika
mashirika mbalimbali likiwemo Redio Tanzania, TBC na yale ya kimataifa kama BBC
na Voa.
0 COMMENTS:
Post a Comment