January 19, 2014





Kiongozi wa zamani wa Simba, Juma Nkamia ametangazwa kuwa Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
 
Nkamia ambaye ni Mbunge wa Kondoa Kusini (CCM),anachukua nafasi ya Amos Makala ambaye amehamia katika wizara nyingine ya maji.

Nkamia aliyewahi kuwa Katibu Mwenezi wa Simba, ametangazwa leo wakati wa baraza jipya la mawaziri ambalo limetangazwa baada ya baadhi ya mawaziri kufutwa kazi na wengine.
Nkamia ambaye taaluma yake ni mwandishi wa habari amewahi kufanya kazi ya utangazaji katika mashirika mbalimbali likiwemo Redio Tanzania, TBC na yale ya kimataifa kama BBC na Voa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic