Mshambuliaji Mcameroon, Samuel Eto’o maarufu kama Shemeji hapa nchini ameweka rekodi mpya ya kufunga mabao matatu.
Chelsea imeichapa Man United kwa mabao
3-1 katika mechi ya Ligi Kuu England iliyopigwa Uwanja wa Stamford Bridge
jijini London.
Bao la ‘kufutia’ hasira la Man United
lilifungwa na Chicharito aliyeingia kipindi cha pili.
Eto'o ambaye baadhi ya wachambuzi wamekuwa wakisema amekwisha au kumalizika kabisa kwa kiwango chake alionekana mwiba kwa mabeki wa United.
Man United walionekana hatari katika
dakika saba za mwanzo, baada ya hapo wakapoteza uelekeo.
Kama Chelsea wangekuwa makini zaidi
wangeweza kushinda zaidi ya mabao hayo.
0 COMMENTS:
Post a Comment