February 5, 2014






MILOVAN NA MWENZAKE WAKIWA WAMESHIKA JEZI ZA MYNMAR

Kocha wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic ameula baada ya kupata ajira mpya ya kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Myanmar.
 
HUYU NDIYE BOSI WA MILOVAN

Milovan amethibitisha kuingia mkataba wa mwaka mmoja na nusu katika nafasi hiyo na tayari yuko nchini humo.

Kocha huyo wa zamani wa Simba atakuwa chini ya kocha mwingine mzoefu, Raddy Avramovic ambaye aliwahi kuwa kocha mkuu wa Singapore mwenye mafanikio makubwa.
 
BENCHI LA UFUNDI LIKIKARIBISHWA NA BOSI WA MFF
Jana kulikuwa na sherehe maalum iliyofanywa na Shirikisho la Soka la Myanmar (MFF) kuwakaribisha makocha wote na benchi zima la ufundi akiwemo Milovan.
“Kweli sasa niko hapa na mambo yamekwenda vizuri, kazi yetu ndivyo ilivyo ni safari kila siku, ila ninafurahi kuwa hapa,” alisema Milovan katika mahojiano na SALEHJEMBE.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic