Mechi ya kufunga Ligi Kuu Bara kati ya
mabingwa, Azam FC dhidi ya JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi
itakuwa bure.
Uongozi wa Azam FC umepeleka ombi lake
kwa Bodi ya Ligi na limekubaliwa kuwa mechi hiyo itakuwa haina kiingilio.
Lengo la Azam FC ni kukabidhiwa kombe na
imewapa nafasi wananchi kujitokeza kwa wingi ili kuishuhudia ikikabidhiwa kombe
la ubingwa wa Ligi Kuu Bara ambalo imelitwaa kwa mara ya kwanza.
Azam imelitwaa kombe hilo baada ya
kuifunga Mbeya City kwa mabao 2-1 katika mechi iliyochezwa mjini Mbeya wiki
iliyopita.
0 COMMENTS:
Post a Comment