April 30, 2014


ALIYEKUWA kipa wa Simba, Mganda, Abel Dhaira (26), anayechezea IB Vestmsnnseryjav ya nchini Iceland kwa sasa, ametua nchini Hispania kwa ajili ya kuweka kambi ya wiki mbili kujiandaa na Ligi Daraja la Kwanza nchini humo.

Dhaira alijiunga na Simba msimu uliopita na kucheza mzunguko wa kwanza kabla ya kutemwa kutokana na kuonyesha kiwango kidogo kwenye ligi.
Akizungumza na gazeti hili, kipa huyo alisema timu yake kwa sasa imehamishia kambi Hispania kutokana na baridi kuzidi nchini Iceland na sasa wanajiandaa vyema kwa ajili ya ligi hiyo.
Dhaira alisema timu yake hiyo inashiriki Ligi Daraja la Kwanza na amefanikiwa kupata namba katika kikosi cha kwanza na maendeleo yake ni mazuri na anaendelea kuongeza bidii zaidi ili atimize ndoto zake za kuwa mchezaji bora.
“Tupo nchini Hispania ambapo tumeweka kambi huku kutokana na kipindi hiki kuwa na baridi kali Iceland, tunashukuru tunaendelea vizuri na maandalizi na lengo letu ni kuhakikisha tunafanya vizuri.

“Lakini kitu muhimu kwangu kwa sasa ni kwamba nimepata namba katika kikosi cha kwanza na naendelea vizuri na timu ipo katika nafasi nzuri kwenye ligi,” alisema Dhaira.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic