June 1, 2014



Kikosi cha timu ya soka ya taifa, Taifa Stars kimesonga mbele na itakutana na Msumbiji katika hatua ya mwisho kuwania kucheza 
makundi ya Kombe la Mataifa Afrika nchini Morocco, mwakani.

Msumbiji imesonga mbele kwa kuwang'oa Sudan Kusini na sasa ni zamu ya kuwavaa Stars.

Stars imewang’oa Zimbabwe baada ya mechi iliyomalizika hivi punde mjini Harare kumalizika kwa sare ya mabao 2-2.
Katika mechi ya kwanza jijini Dar es Salaam, Stars ilishinda kwa bao 1-0 lililofungwa na John Bocco.
Lakini katika mechi ya leo, kazi haikuwa lelemama baada ya wenyeji Zimbabwe kupata bao mapema katika dakika ya 12 kupitia kwa Danny Phiri.
Lakini Stars chini ya Mart Nooij ikasawazisha katika dakika ya dakika ya 26 kupitia Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
Kipindi cha pili kiliponza tu, Thomas Ulimwengu akaongeza la pili katika dakika ya 46 na dakika ta 55, Willard Katsande akaisawazishia Zimbabwe.
Pamoja na juhudi za mwamuzi wa mchezo huo kuongeza dakika 7 za nyongeza, lakini bado mambo yalikuwa magumu kwa wenyeji na matokeo hayakubadilika.
Hivyo Stars imesonga mbele kwa jumla ya mabao 3-2 na inasubiri makundi sasa.
Timu nyingine za Afirka Mashariki zimesonga mbele ambazo ni Kenya, Uganda na Rwanda ambayo iliitungua Libya kwa mabao 3-0.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic