July 16, 2014



Mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, kutoka nchini Brazil, Andrey Coutinho, jana aliwapiga darasa washambuliaji wa timu hiyo, Jerry Tegete na Hussen Javu, akiwaonyesha jinsi wanavyotakiwa kupokea mpira wanapokuwa ndani ya eneo la hatari.

Coutinho ambaye sasa ana wiki mbili tangu ajiunge na Yanga, alifikia hatua hiyo, baada ya washambuliaji hao mara kwa mara kushindwa kumalizia kwa ustadi mkubwa mipira ya krosi ambayo alikuwa akiwapigia, wakati wa mazoezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari Loyola, Mabibo jijini Dar es Salaam.

Kutokana na hali hiyo, Coutinho alilazimika kuwaonyesha wachezaji hao jinsi ya kuzitumia nafasi hizo kwa kutumia kichwa kuunganisha krosi hizo alizokuwa akiwapigia, lakini pia pale wanapoona hawawezi watumie kifua kumiliki mpira.

Hata hivyo, Tegete na Javu walionekana kumuelewa mchezaji huyo na kuufanyia kazi ushauri wake na baada ya muda, wakafanikiwa kuzifumania nyavu.

Hata hivyo, baada ya hali hiyo, kocha mkuu wa timu hiyo, Mbrazili Marcio Maximo, alilazimia kuwakusanya wachezaji wote na kuwapa mazoezi ya kufunga wakiwa nje ya eneo la hatari kwa kugongeana pasi mbili kisha kupiga shuti langoni.
SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic