July 16, 2014



Kiwango cha juu anachoonyesha mazoezini kipa wa Yanga, Juma Kaseja, kimemvutia zaidi kocha mkuu wa timu hiyo, Mbrazili, Marcio Maximo, hali ambayo inamweka kwenye wakati mgumu aliyekuwa kipa chaguo la kwanza, Deogratius Munishi ‘Dida’, ambaye sasa yupo na timu ya taifa, Taifa Stars.
Dida kwa sasa yupo Tukuyu mkoani Mbeya na kikosi cha Taifa Stars, kilichopiga kambi yake huko kujiandaa na mechi ya kimataifa ya kutafuta tiketi ya kufuzu kwa Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Msumbiji.

Hali hiyo imemfanya Kaseja ambaye yupo na kikosi cha Yanga kinachoendelea na mazoezi yake ya kujiandaa na msimu ujao wa ligi kuu, kuzidi kujifua mbele ya Maximo ili aweze kujitengenezea mazingira mazuri yatakayomfanya awe kipa chaguo la kwanza.

Kocha wa makipa wa Yanga, Juma Pondamali, ameliambia gazeti hili kuwa, Dida atakaporudi katika kikosi hicho, atakuwa na kazi kubwa ya kufanya ili aweze kumshawishi Maximo kama ilivyo sasa kwa Kaseja ambaye anaonyesha kiwango kizuri mazoezini.

“Binafsi nawaamini makipa wote watatu wa kikosi chetu ambao ni Kaseja, Dida na Barthez (Ally Mustapha), wana uwezo wa juu.

“Lakini ili waweze kupata nafasi katika kikosi cha Maximo, inabidi wapambane na hivi sasa Kaseja anaendelea vizuri, hivyo Dida atakaporejea kutoka timu ya taifa, anatakiwa kuonyesha kuwa anaweza.

“Kama akisinzia basi wenzake wanaweza kumshusha kwa sababu wanafanya vizuri hivi sasa mazoezini,” alisema Pondamali.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic