July 18, 2014



Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe ndiye anasubiriwa ili kumaliza suala la mkataba wa Kocha Zdravko Logarusic.


Loga alianza majadiliano na Hans Poppe mara tu baada ya mwisho wa msimu uliopita.

“Hivyo tunalazimika kumsubiri mwenyekiti wa kamati ya usajili ili kumaliza zoezi hilo,” alisema Said 
Tully ambaye ni mmoja wa wajumbe wa kamati ya usajili.

“Akiwepo Hans Poppe na sote pamoja, itakuwa lahisi kujua walianza vipi, walifikia wapi na itakuwa lahisi kulijadili na kulimaliza.

“Hivyo kwa pamoja tutavuta subira kidogo na kumsubiri Hans Poppe, atakapokuja basi tutalifanyia kazi suala hilo ili lifikie mwafaka,” alisema Tully.
Loga bado hajasaini mkataba mpya na zoezi hilo huenda likakamilika baada ya siku mbili atakapokuwa amerejea mwenyekiti huyo.
Kocha huyo Mcroatia aliifundisha Simba kwa nusu msimu na baadaye akarejea kwao Croatia kwa mapumziko.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic