July 18, 2014



Uongozi wa klabu ya Simba kupitia kamati yake ya usajili umeanza kazi ya kusaka viungo wawili na mshambuliaji mmoja ili ifunge usajili.
Simba imeanza kazi hiyo mara moja baada ya Kocha Zdravko Logarusic kusisitiza nataka watu wa kazi kwelikweli.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba zimeeleza, kamati ya usajili imeanza zoezi hilo ikiendelea kuitumia ripoti ya kocha huyo.
“Kazi imeanza haraka na ndani ya siku chache tutakuwa tumewapata viungo hao, lengo ni kukamilisha ripoti ya kocha,” kilieleza chanzo.

Tayari Simba imefanya usajili wa zaidi ya wachezaji watatu kwa lengo la kujiimarisha na moja ya pendekezo la Logarusic ilikuwa ni nafasi ya kipa na Simba imemsajili Hussein Sharrif ‘Cassilas’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic