Mama mzazi wa Cristiano
Ronaldo amejikuta akimwaga machozi wakati akielezea namna alivyotaka kuitoa
mimba ya mwanaye huyo ambaye ni staaa.
Dolores Aveiro ameyasema hayo
nchini Ureno wakati akizindua kitabu chake na kuhadithia kwamba daktari ndiye
alikataa kuitoa mimba ya Ronaldo.
Kutokana na daktari kukataa,
Dolores alirudi nyumbani na kunywa bia ya moto halafu akafanya mazoezi makali
na lengo lilikuwa ni kuona mimba hiyo inatoka.
“Lakini siku moja Ronaldo
alijua kuhusiana na hilo, akanieleza maneno yaliyoniuma sana, kwamba nilitaka
kuitoa mimba yake lakini yeye ndiye rafiki na msaada kwangu,” alisema Dolores.
Ronaldo anayekipiga Real
Madrid ana kaka yake pamoja na dada wawili na wamekuwa wakiishi kwa umoja na
ushirikiano wa karibu sana.
|
0 COMMENTS:
Post a Comment