LOGA AKIWA KWAO CROATIA |
Kocha Mkuu wa
Simba, Zdravko Logarusic amesema yuko tayari kwa kazi na atatua nchini wakati
wowote ndani ya wiki hii.
“Wakati wowote
nitakuwa Tanzania, mapumziko yameisha na akili yangu imehamia kwenye kazi.
“Kila kitu
ninachowaza kwa sasa ni Simba tu, najielewa kuwa mapumziko yamkwisha,” alisema.
Loga alikuwa
kwao Croatia kwa mapumziko na pia alifanya ziara nchini Bosnia-Herzegovina kwa
ajili ya kujipumzisha.
Simba
inatarajia kuanza mazoezi wiki hii, imeelezwa baada ya hapo itakwenda kuweka
kambi mjini Zanzibar.
0 COMMENTS:
Post a Comment