Na Saleh Ally
BURUDANI ya Kombe la Dunia hata kama ni
utamu, basi ndiyo ule unatoweka mdomoni kama mtu aliyeanza kutafuna Big G,
baada ya muda, kutafuna kunabaki fasheni tu, utamu unakuwa umepotea.
Uzuri ni kitu kimoja, kila baada ya utamu
huu, unafuatia ule. Baada ya Kombe la Dunia, sasa macho, masikio yanaelekezwa
upande mwingine, ligi za nchi mbalimbali.
Unapoangalia ligi za nchini mbalimbali ni
vigumu sana kuanzia kwingine, hauwezi kukwepa Ligi Kuu England maarufu kama
Premiership.
Ina mengi ya kujifunza ambayo kwa wale
wanaoshiriki Ligi Kuu Bara, mfano Bodi ya Ligi, Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF), viongozi wa klabu, makocha, wachezaji na hata mashabiki wanaweza
kujifunza.
Msimu uliopita watu milioni 13.9, unaweza
kusema milioni 14 walishuhudia mechi 380 za Premiership. Wastani wake ni
watu 36,657 kwa mechi moja. Hapa
tu unaweza kujifunza kuwa kwa ligi yetu nyumbani wameingia watu wangapi.
Idadi ya watu milioni 14, maana yake ni
zaidi ya raia wote wa Rwanda, ndiyo waliingia viwanjani kushuhudia mechi za
ligi hiyo. Nakuhakikishia, asilimia 2 au 3 watakuwa ni Watanzania wanaosafiri
hadi Uingereza kushuhudia mechi za ligi hiyo.
Hawafuati kingine, badala yake ni burudani
inayoridhisha mioyo yao, ndiyo maana utajiri mkubwa unazidi kuongezeka katika
ligi hiyo, kwa kuwa watu kibao kutoka mataifa katika Bara la Afrika, Asia na
kwingineko wamekuwa wakitoa fedha zao kwenda England.
Lazima kuwe na hamu ya mafanikio hata kwa
kiwango cha chini lakini watu kuingia kwa wingi uwanjani, lazima kuwe na
viwanja bora, sehemu ya kukaa na kuchezea. Timu pia zionyeshe soka safi
litakalowavuta wengi.
Haya yanawezekana kama kukiwa hakuna
migogoro, watu wenye tamaa za kushibisha matumbo yao badala ya mafanikio ya
soka lenyewe na ikiwezekana makomandoo wote ‘wafe’ ili soka lipande kwa kuwa
England hakuna hata mmoja soka linaendelea.
Maneno mengi ya nini! Taratibu kwa wakati
wako soma takwimu za Premiership msimu uliopita, uone utamu wake na huenda
msimu ujao zikapanda. Je, hapa nyumbani tunazo takwimu za kutuonyesha na
tunajua kuwa tunapanda au tunateremka? Hodi England.
MSIMU WA 2013–14
Mabingwa: Man City
Mechi zilizochezwa: 380
Mabao yaliyofungwa:
1052 (mabao 2.77 kwa mechi)
Mfungaji Bora: Luis Suarez (mabao 31)
Kipa Bora: Petr Čech & Wojciech Szczęsny
(wote mechi 16 bila kufungwa)
Ushindi mkubwa nyumbani: Man City 7–0
Norwich
Ushindi mkubwa ugenini: Tottenham 0–5
Liverpool
Mechi zenye mabao mengi: Man City 6–3
Arsenal
Cardiff City 3–6 Liverpool
Ushindi mfululizo: Liverpool
(Liverpool-mechi 11)
Mechi nyingi bila kufungwa: (Liverpool-mechi
16)
Mechi nyingi bila kushinda:
(Fulham&Sunderland, Wes Brom-mechi 9)
Vipigo vingi mfululizo: (Crystal
Palace-Mechi 7)
Watu wengi uwanjani: 75,368 (ManU 4–1 Aston
Villa)
Watu wachache uwanjani: 19,242 (Swansea 3–3
Stoke)
Jumla ya walioona Premiership viwanjani: 13,929,810
Wastani kwa mechi: 36,657








0 COMMENTS:
Post a Comment