July 19, 2014




Uongozi wa timu ya Mbeya City ya Mkoani Mbeya, imesogeza mbele tarehe ya kuanza mazoezi kufuatia kusogezwa mbele kwa ligi kuu.


Awali timu hiyo ilikuwa iingie kambini Julai 19 tayari kwa kuanza maandalizi ya msimu ujao wa ligi kuu lakini wameamua kubadilisha kufuatia kusogezwa mbele kwa ligi hiyo ambayo sasa itaanza Septemba 20.

Katibu Mkuu wa Mbeya City, Emannuel Kimbe ameeleza kuwa kikosi chao kinatarajia kuingia kambini Agosti 15 kwa ajili ya kuanza maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu Bara.
“Tumeamua kusogeza mbele tarehe ya kungia kambini kufuatia TFF kusogeza mbele ligi, hivyo tunatarajia kuingia kambini Agosti 15 au 16 kwa ajili ya kuanza maandalizi ya msimu mpya.
“Kuhusu mechi za kirafiki kocha ndiye atakayeamua anahitaji ngapi na sisi kama uongozi tutafanya utekelezaji kufuatia maombi yake,” alisema Kimbe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic