| MAGORI AKIZUNGUMZA NA WACHEZAJI WA YANGA.
Mkurugenzi wa uendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya
Taifa (NSSF), Crescentius Magori amewapa daraja la kutosha wachezaji wa Yanga.
Magori ambaye ni mjumbe wa kamati ya usajili ya
Simba alitoa darasa hilo leo akiwaelezea wachezaji wa Yanga umuhimu wa kukopa
nyumba bora za NSSF.
Pamoja na wachezaji hao, Magori alitoa darasa
kwa Kocha Mkuu Marcio Maximo pamoja na wasaidizi wake.
Wachezaji hao walipata nafasi ya kumuuliza
maswali bosi huyo wa NSSF ambaye aliyajibu kiutaalamu hadi wote waliporidhika.
Wachezaji wa Yanga wanaruhusiwa kukopa nyumba
katika maeneo ya Kijichi na Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
Yanga inakuwa klabu ya kwanza nchini kuwafanyia
wachezaji wake na staff wa benchi la ufundi mpango huo mzuri unaojali maisha
yao ya sasa na baadaye.
|
0 COMMENTS:
Post a Comment