Beki Rio Ferdinand amesaini
kuichezea Queen Park Rangers ambayo imerejea Ligi Kuu England.
Timu hiyo maarufu kama QPR kutoka
Loftus Road imekamilisha usajili huo na kumnasa mkongwe huyo wa zamani wa Man
United.
Rio atalamba mkataba wa
miezi 12 tu, yaani mwaka na atakuwa akichukua kitita cha pauni 70,000 kwa wiki.
Awali Rio alionekana kutaka
kubaki Man United na kucheza kwa msimu mmoja zaidi, lakini akatolewa nje.
Wengi hawakuamini
angeondolewa katika hatua za mwisho na baadaye alilaani na kudai ilichangia kwa
kuwa asili yake ni Peckham, London na si kijana wa Manchester kama ilivyo kwa
akina Paul Scholes, Ryan Giggs na wengine.








0 COMMENTS:
Post a Comment