August 15, 2014



Kocha maarufu nchini Charles  Boniface Mkwasa amerejea nyumbani na kusema yuko huru kumfundisha timu yoyote inayomhitaji.
Mkwasa amerejea nyumbani baada ya mkataba wake na klabu ya Al Shaollah FC ya Saudi Arabia kuvunjwa ghafla.
Mkwasa alikuwa msaidizi wa Hans van der Pluijm na wote mikataba yao ilivunjwa.

Akizungumza jijini Dar, kocha huyo na mchezaji wa zamani wa Yanga amesema yuko tayari ;kudaka’ kazi itakayojitokeza mbele yake.
 “Nimerejea nyumbani, nitapumzika kidogo ila kama kuna timu itanihitajia kuweza kufanya nao kazi  sina tatizo katika hilo, tutafanya kikubwa ni maelewano,” alisema Mkwasa.
Aidha, Mkwasa alisisitiza lijifunza mengi licha ya kufanya kazi Saudi kwa kipindi kifupi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic