Kocha maarufu nchini Charles Boniface Mkwasa amerejea nyumbani na
kusema yuko huru kumfundisha timu yoyote inayomhitaji.
Mkwasa alikuwa msaidizi wa Hans van der Pluijm
na wote mikataba yao ilivunjwa.
Akizungumza jijini Dar, kocha huyo na mchezaji
wa zamani wa Yanga amesema yuko tayari ;kudaka’ kazi itakayojitokeza mbele
yake.
“Nimerejea
nyumbani, nitapumzika kidogo ila kama kuna timu itanihitajia kuweza kufanya nao
kazi sina tatizo katika hilo,
tutafanya kikubwa ni maelewano,” alisema Mkwasa.
Aidha, Mkwasa alisisitiza lijifunza mengi licha
ya kufanya kazi Saudi kwa kipindi kifupi.
0 COMMENTS:
Post a Comment