August 15, 2014



Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema litafanya uchunguzi kujua uhakika wa deni unalodaiwa na kampuni ya kutengeneza tiketi ya nchini Kenya.
TFF ilikuwa inadaiwa Sh milioni 140, lakini inaelezwa imelipa Sh milioni 70 na bado basi lake aina ya Youtong linashikiliwa kutokana na deni hilo.
Wambura amesema watafanya uchunguzi, lakini akasisitiza, uchache wa watu wenye baadhi ya mechi kimekuwa chanzo cha deni hilo.
“Unajua kuna wakati mechi zinakuwa na watu wachache sana, lakini wenyewe wame-supply tiketi tu.
“Hivyo ni lazima ulipe na utaona mechi kadhaa zikiwa namna hiyo, deni linaongezeka kwa kuwa mechi hizo zinakuwa hazilipi.
“Kuna mambo ya kuangalia lakini tunaendelea kujitahidi kiasi kilichobakia kimalizike,” alisema Wambura.
Wadau wa soka wameonyesha kushangazwa na taarifa za kukamatwa kwa basi hilo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic