September 23, 2014

CHIPPO
Kocha Mkuu wa Coastal Union, Yusuf Chippo amesema kikosi chake kipo tayari kupambana mjini Mbeya na kinataka kurejea Tanga na pointi zote tatu.

Chippo raia wa Kenya amesema kikosi chake kinataka kurejea na pointi tatu katika mechi yao ya pili ambayo watacheza mjini Mbeya.
“Tuko njiani, tunatarajia kuwasili Mbeya hivi karibuni. Tumeamua kwenda mapema na hii ni mipango ya timu,” alisema Chippo.
Alipoulizwa hana hofu ya kupoteza pointi zote tatu kwa kuwa Mbeya City hawatataka kufanya mchezo baada ya mechi ya kwanza kubanwa kwa sare ya bila mabao na JKT Ruvu, akasema.
“Hatuna majeruhi, hatuna tatizo lolote na tuko tayari kwa vita. Hatutajali wao wanawaza nini lakini sisi ni kupambana na kujituma, tunachotaka ni kushinda.”
Coastal Union ilianza ligi hiyo kwa sare ya ugenini dhidi ya Simba ikisawazisha mabao mawili katika kipindi cha pili baada ya wenyeji wao kuongoza kwenye Uwanja wa Taifa kwa mabao mawili hadi mapumziko.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic