September 23, 2014

Kiungo nyota wa Yanga, Andrey Coutinho amerejea katika kiwango chake safi kabisa na sasa ataanza kuichezea Yanga dhidi ya Prisons ya Mbeya kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, Jumapili.

Coutinho aliikosa mechi ya ufunguzi ya Ligi Kuu dhidi ya Mtibwa Sugar mjini Morogoro, Jumamosi ijayo kutokana na kuwa majeruhi.
Lakini tayari raia huyo wa Brazil sasa yuko fiti baada ya kucheza mechi mazoezi leo.
“Kweli Coutinho sasa amerejea vizuri na suala la kumtumia linabaki kwa mwalimu mwenyewe.
“Unajua kawaida, uongozi wa Yanga hautaki kuingilia masuala ya mwalimu lakini Coutinho amepona,” alisema Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu.

Mashabiki wa Yanga walikuwa na hamu kubwa kumuona kiungo huyo mwenye kasi na chenga za maudhi akiichezea timu yao kwa mara ya kwanza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic