September 24, 2014

CHANONGO (KULIA) AKIPAMBANA

Baada ya Simba kuwa na uhakika sasa itamkosa mshambuliaji wake Paul Kiongera katika mechi dhidi ya Yanga, sasa mwingine tena, Harun Chanongo ataikosa mechi ya Jumamosi.

Simba inashuka dimbani Jumamosi kuwavaa Stand United ya Shinya.
Taarifa zinaeleza, Chanongo ataanza mazoezi mepesi Alhamisi au Ijumaa, hivyo itakuwa vigumu kucheza mechi ya Jumamosi.
Hivyo kocha Patrick Phiri atalazimika kumtumia mchezaji mwingine, huenda nafasi hiyo akaichukua mkongwe Amri Kiemba.
Chanongo pia aliumia katika mechi dhidi ya Coastal Union na anatakiwa kupumzika siku nne.
Uhakika unaeleza itakuwa vigumu kuwavaa Stand kutokana na maumivu aliyokuwa nayo kuhitaji mazoezi ya taratibu angalau siku nne nyingine.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic