Udhamini wa kampuni maarufu ya kuuza matairi, lim na betri za
magari ya Bin Slum, imewapa neema mpya Stand United.
Stand United sasa imepata udhamini kutoka kwa benki ya Exim tawi
la mkoa wa Shinyanga.
Ingawa haikuwekwa wazi, benki hiyo itatoa kiasi cha fedha na
kutengeneza vifaa vya michezo.
Exim imeingia baada ya kampuni ya Bin slum kuidhamini timu hiyo
kupitia matairi yake ya Double Star.
Hali hiyo imewaamsha baadhi ya wadhamini na kuamua kuingia
kuidhamini kwa ajili ya Ligi Kuu Bara.
Timu hiyo ikiwa nyumbani imeanza kwa kipigo cha mabao 4-1, hivyo
itakuwa changamoto kwake kujitahidi ili kuwainua wadhamini na mashabiki wake.
0 COMMENTS:
Post a Comment