October 8, 2014


Klabu ya Azam FC, imekuwa kinara wa kuwa na wachezaji wengi kwenye timu ya taifa, Taifa Stars, baada ya wachezaji wake kumi kuitwa kwenye timu hiyo.


Stars inajiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya Benin utakaopigwa Oktoba 12 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Wachezaji ambao wameitwa katika kikosi cha timu ya taifa kutoka katika klabu hiyo ni pamoja na mabeki Said Moradi, Aggrey Morris, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni na Gadiel Michael, viungo ni Salum Abubakar ‘Sureboy’ Himid Mao na Mcha Khamis na makipa Mwadini Ali na Aishi Manula.
Wachezaji kutoka Yanga ni saba na Simba ni wanne pekee na mmoja kutoka Mbeya City pamoja  na wale wanne ambao wanacheza nje ya nchi.

Akizungumza na Championi Jumatano, Ofisa Habari wa Azam, Jaffar Idd, alisema kuwepo kwa wachezaji 10 katika timu ya taifa ni wazi kuwa kikosi chao ni bora  na hicho kinazidi kuwapa matumaini ya kuendelea kupigana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic