October 8, 2014

STAND UNITED, IMEPANDA MSIMU HUU.

Timu nne zinatarajiwa kupanda Ligi Kuu Tanzani Bara msimu ujao huku timu mbili pekee msimu huu zikishuka daraja ili kuweza kuandaa mpango mpya wa msimu wa mwaka 2015/2016, ambapo timu 16 ndizo zitakazoshiriki ligi hiyo.

 Kwa sasa ligi kuu ina timu 14 pekee, ambazo zinashiriki na kila msimu zilikuwa zikishuka timu tatu pekee na kupanda tatu kutoka daraja la kwanza.
Ofisa Mtendaji wa Bodi ya Ligi, Silas Mwakibinga, amesema kuwa msimu ujao ni timu nne kutoka daraja la kwanza ndizo zitakazopanda na msimu huu mbili zitashuka.
Mwakibinga alisema mpango huo utaanza msimu ujao na kwa sasa waliopo daraja la kwanza wanatakiwa kuonyesha bidii kwa kiasi kikubwa kuhakikisha wanafanikiwa kupanda.

“Timu nne msimu ujao ndizo zitakazopanda ligi kuu na mbili msimu huu ndizo zitakazoshuka, bidii na uwezo wako wa kupata pointi kihalali ndiyo vitakufanya kutoka chini kuja juu na wengi itawabidi warudi huku chini na kujipanga upya,” alisema Mwakibinga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic