Mshambuliaji Diego Costa anayeongoza kwa mabao kwenye Ligi Kuu England, sasa
yuko tayari kwa ajili ya kuanza kuifungia mabao timu yake ya taifa ya Hispania.
Hispania ina kibarua kigumu
wikiendi hii katika mechi ya kuwania kucheza Kombe la Mataifa ya Ulaya ya mwaka
2016 dhidi ya Slovakia.
Tayari kikosi cha Hispania
kimetua mjini Luxembourg na mazoezi aliyofanya Costa akiwa na kikosi hicho,
imeonekana tatizo lake la nyama limepona.
Kama limepona, lazima kocha
Vicente del Bosque ataanza na mshambuliaji huyo.
Wengine alioungana nao
katika kikosi hicho wakitokea Ligi Kuu England ni Cesc Fabregas wa Chelsea, David Silva kutoka Man
United na kipa David de Gea kutoka Man United.








0 COMMENTS:
Post a Comment