Siku
moja baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kumshitaki mwanasheria Dk Damas
Ndumbaro kwenye kamati ya nidhamu, yeye ameibuka na kusema anaona kilichofanywa
na shirikisho hilo ni maajabu ya karne.
Dk
Ndumbaro amesema anaona ni maajabu kwake kushitakiwa kwa ajili ya kuwatetea
wateja wake ambao ni klabu za Ligi Kuu Bara.
“Sijawahi
kusikia wala haijawahi kutokea kusikia mwanasheria anashitakiwa kwa ajili ya
kuwatetea wateja wake.
“Mimi
ni mwanasheria nah ii ndiyo kazi yangu, sasa nashangazwa kushitakiwa kwa ajili
ya kuwatetea wateja wangu, hiki ni kitu cha ajabu kabisa.
“Lakini
nimeaandikia barua TFF kuwaeleza sitaweza kuhudhuria kikao hicho cha kamati ya
nidhamu kesho kwa kuwa ninaondoka kwenda nchini Marekani kutokana na mwaliko wa
chuo kikuu kimoja huko.
“Nitakuwa
nikitoa mafunzo kwa siku Oktoba yote, lakini bado ninataka kujua ninashitakiwa
kwa ajili ya nini na nani,” alisema Dk Ndumbaro akionyesha kujiamini katika
hilo.
“Katika
barua niliyopewa na TFF haielezi nani anayenishitaki, pia haielezi kosa langu
zaidi ya kusema mambo niliyoyazungumza. Yapi.”
Dk
Ndumbaro ndiye mwanasheria anayezitetea klabu za Ligi Kuu Bara ili kuepuka TFF
kuzikata asilimia 5 kwenye udhamini wa Vodacom na Azam TV.
Pia,
Serikali imeishaagiza suala hilo kusitishwa hadi hapo bodi ya ligi na TFF
zitakapokutana Jumamosi na kujadiliana, zifikie mwafaka halafu zirudi
serikalini.








Ndumbaro anawatetea nani wakati Simba na Yanga zimekana kumtambua?Acha uzushi wewe Saleh!
ReplyDeleteTFF inaleta ukoloni wakati nchi imeshapata uhuru, haiwezekani taasisi ikatoa maamuzi yanayowaathiri wadau wake kwa namna yoyote ile bila kuwahusisha, tena bila haki ya wao kuhoji..! huo ni upuuzi usiovumulika wala kukubalika...!
ReplyDelete