Kikosi cha African Sports kimeshinda kwa
bao 1-0 dhidi ya Majimaji na sasa ni pointi moja tu kurejea Ligi kuu Bara.
African Sports inayodhaminiwa na kampuni ya
Bin Slum Tyres Ltd imepata ushindi huo muhimu leo kwenye uwanja wake wa
nyumbani wa Mkwakwani mjini tanga.
Mechi ijayo itakuwa ni dhidi ya JKT Mlale
na iwapo watapata ushindi basi watakuwa wamejihakikishia kupanda daraja.
African Sports wana pointi 41 na
wanafuatiwa na Majimaji yenye pointi 35 na Lipuli ina pointi 35 na kila timu
kati ya hizo zimebakiza mechi tatu.
0 COMMENTS:
Post a Comment