January 19, 2015


Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic amesema kikosi chake sasa ni suala la kazi mbele na hakutakuwa na sherehe yoyote kufurahia ubingwa wa Kombe la Mapinduzi.


Akizungumza mjini Dar es Salaam, Kopunovic amesema ushindi wa Kombe la Mapinduzi na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ndanda FC katika Ligi Kuu Bara, hahitaji kuona watu wanasherekea.

“Kama unaulizia sherehe haitakuwepo, watu kadhaa wameniuliza kuhusiana na hilo lakini hakuna sababu ya kufanya hivyo.

“Walijua baada ya kutoka Mtwara tutafanya sherehe. Imeishapita, tumeshinda na sasa ni tunatengeneza timu kwa ajili ya mechi nyingine.

“Kuifunga Ndanda hakikuwa kitu lahisi, wala usidhani tumeshinda kwa kushitukiza au mimi sijui,” alisema Kopunovic raia wa Serbia na kuongeza.
“Nimefundisha Rwanda kwa miaka mitatu, najua mechi za ugenini zinavyokuwa ngumu. Najua unapokuwa na timu kubwa timu nyingine zinapoikamia, hivyo tulijipanga.

“Kawaida ushindi mmoja unachangia watu kukukamia zaidi, hivyo tunatakiwa kujipanga zaidi ndiyo maana sioni sababu ya kuwa na sherehe.”


MSerbia huyo aliyechukua nafasi ya Patrick Phiri kwa kushirkiana na msaidizi wake Selemani Matola wameiwezesha Simba kubeba Kombe la Mapinduzi lililoshirikisha timu mbalimbali zikiwemo Yanga, Azam FC, Mtibwa Sugar, Polisi Zanzibar, KMKM, Shaba, JKU na waliokuwa mabingwa watetezi KCCA ya Uganda.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic