January 25, 2015

NDANDA FC.
Kagera Sugar imepoteza mechi ya tatu mfululizo katika Ligi Kuu Bara baada ya kuchapwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wake wa 'nyumbani' wa CCM Kirumba mjini Mwanza.

Ndanda FC ndiyo waliokuwa wababe wa Kagera Sugar leo baada ya kuonyesha soka zuri na la kuvutia hasa katika kipindi cha pili.

Kocha wa Kagera Sugar, Jackson Mayanga amesema kuwa ma majeruhi wengi kumechangia wao kuendelea kuboronga kwenye dimba la Kirumba.

Kagera imekuwa ngangari kweli kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Kaitaba mjini Bukoba.

Mechi nyingine ilikuwa kati ya JKT Ruvu imemaliza kwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Mgambo katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar..


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic