Baada ya kiungo wa Yanga, Andrey Coutinho, raia
wa Brazil, kuonyesha nia yake ya kuichezea timu ya taifa ya Tanzania, Taifa
Stars, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limemkubalia lakini limempa masharti
ya kufuata.
Coutinho aliyetua Yanga mwanzoni mwa msimu huu,
alitamka kuwa kutokana na nafasi finyu ya yeye kuichezea timu ya taifa ya
nchini kwao, basi yupo tayari kuichezea Taifa Stars kama TFF itamhitaji afanye
hivyo.
Katibu wa TFF, Selestine Mwesigwa, amesema kuwa
hakuna kifungu chochote ndani ya shirikisho hilo kitakachomzuia kuichezea
Stars, lakini anatakiwa kwanza kubadili uraia na siyo shirikisho kuhangaika
kumbadilishia.
“Sisi
hatumzuii ila kama anahitaji hivyo inatakiwa yeye mwenyewe abadili uraia na
siyo sisi kumbadili, kingine pia kocha wa timu ya taifa, Martin Nooij ndiyo
mwenye maamuzi ya mwisho kama akishabadili atutaarifu ili tufahamu, kama kocha
akivutiwa na kiwango chake na akichaguliwa basi tumjumuishe kwenye kikosi,”
alisema Mwesigwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment