January 20, 2015


Uongozi wa klabu ya Yanga umeshauri timu za majeshi kupewa nafasi ya kushiriki Ligi Kuu Bara ya wanajeshi.



Msemaji na mkuu wa kitengo cha Yanga, Jerry Muro amesema timu za majeshi zimekuwa zikigeusa mchezo wa soka kama vita.

"Kweli ile ni vita na si jambo jema. Hivyo tunawaomba kama TFF wataweza basi wawape nafasi watu hawa kucheza ligi yao.

"Wacheze timu za majeshi maana wao watakuwa wana mbinu za kijeshi kupambana. Sisi raia hatuwezi, wanaweza wakatuua," alisema Muro.

"Ukiangalia tukio la yule beki wa Ruvu Shooting akimkaba Tambwe utagundua hakuna tena uungwana katika soka."

Picha iliyochapishwa katika gazeti bora la michezo la CHAMPIONI imezua gumzo kubwa katika mitandao mbalimbali nchini.

Picha hiyo inamuonyesha beki George Michael akimkaba Tambwe kikatili huku akiwa anavuja damu mdomoni.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic