February 25, 2015


Azam FC imeondoka nchini  jana, Saa 2:30 Usiku kwa Ndege ya Shirika la Kenya (Kenya Airways) kuelekea nchini Sudan tayari kwa  kujiandaa na mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika  dhidi ya El Merreikh.


Azam wanaondoka wakiwa na pigo kwa kuwa watawakosa wachezaji wao mahiri watatu Kipre Balou, Mudathir Yahaya na Wazir Salum ambao wana matatizo tofauti.

Usajili wa Mudathir unaonekana kuwa na matatizo huku Kipre na Salum wakisumbuliwa na majeraha.

Mechi ya mabingwa hao wa Tanzania Bara itapigwa Jumamosi saa 2 usiku.

Huu utakuwa mchezo wa pili kwa timu hizo kukutana baada ya awali kuvaana kwenye Uwanja wa Chamazi na vijana hao wa Tanzania wakaibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Katibu wa Azam FC, Idrissa Nassor amesema kuwa kikosi cha timu hiyo kimeondoka nchini jana na wachezaji 21, huku wengine watatu wakishindwa kuondoka kutokana na kuwa na matatizo tofauti.

 “Timu inatarajia kuondoka leo (jana), saa mbili usiku kwa Ndege ya Shirika la Kenya, kuelekea Sudan ambapo tutaondoka na wachezaji 21 kati ya 24, tuliowasajili ambapo watatu kati yao hawatakwenda kutokana na matatizo mbalimbali.

“Kuhusu Kavumbagu, paspoti yake ilikuwa imejaa hivyo alilazimika kurejea kwao Burundi kuirekebisha, tayari amesharejea na atakuwa miongoni mwa wachezaji watakaokwenda.


“Tumejiandaa vizuri na kitu chochote kitakachotokea kwani na sisi tuna akili timamu kama kuna hujuma yeyote ile ambayo itatokea tutajua jinsi ya kukabiliana nayo,” alisema Nassor.

1 COMMENTS:

  1. Tunaomba Mungu awaepushe na maovu yao,tunawaombea ushindi tena.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic